Ujumbe kwa mtangazaji
Maji ni ya muhimu na ni moja kati ya mahitaji muhimu kwa uhai wa binadamu, na kwa kawaida yanalinganishwa na “uhai.” Hata hivyo, upatikanaji na salama wake ni vitu viwili muhimu kwa ajili ya maisha bora. Unatikanaji wa maji safi ni jambo muhimu sana hasa katika kipindi hiki tunapokabiliana na matatizo ya mabadiliko ya tabia nchi. Katika maeneo mengi, hasa vijijini, maji kidogo yanayopatikana huko, mara nyingi huwa sio safi na yanapatikana umbali mrefu kutoka katika makazi ya wanakijiji. Watoto ndio waathirika wakubwa wa hali hii. Uhaba wa maji, na mazingira machafu, mara nyingi husababisha maradhi na vifo na hata vifo kwa watoto kutokana na magonjwa ya kuharana na magonjwa mengine yanayotokana na uchafu.
Wanawake, na kwa kiasi Fulani watoto, wanawajibu wa kutafuta maji kwa matumizi ya nyumbani, kuyatoa toka pale yanapopatikana hadi nyumbani, kuyatunza hadi pale yatakapotumika, kuyatumia kupikia, kufanyia usafi, na kunyweshea mifugo nyumbani. Kunapokuwa na upungufu wa maji, wanaoteseka ni wanawake na watoto, ambapo inawalazimu kutumia saa sita kwa siku wakitembea kutafuta maji, ambayo yanaweza kuwa sio salama. Ni vema watangazaji wakatambua tatizo hili na kutangaza kuhusu uhifadhi wa maji safi.
Muswada huu kutoka nchini Tanzania unaonyesha juhudi za pamoja za wakulima kijijini katika eneo lenye upungufu wa maji tangu kijiji hicho kilipoanzishwa miaka ya 1960. Hakuna vyanzo vya maji kijijini; wanawake na watoto (hasa wa kike) wanatembea umbali wa kilometa nane kutafuta maji. Maji yanayochotwa si salama, kwa sababu chanzo cha maji ni bwawa tu lililochimbwa ardhini ambalo maji yake hujikusanya wakati wa mvua. Kwa vile bwawa hili linatumiwa na mifugo kunywa maji, mara kadhaa mifugo huingia ndani na kuchafua maji. Magonjwa yanayotokana na uchafu wa maji yamekuwa ni ya kawaida kijijini hapo.
Baada ya kuteseka kwa miaka mingi, wakisubiri serikali kuwapatia maji, wanakijiji kwa pamoja waliamua kutatua tatizo lililokuwa linawakabili. Walichimba bwawa kuvuna maji wakati wa masika. Wanaweza kutumia maji haya ya kwenye bwawa kwa miezi mitatu baada ya msimu wa mvua kumalizika. Pia serikali ya kijiji inakusanya fedha kutoka kwa wanakijiji kulipia gharama za uchimbaji wa visima ili waweze kupata maji safi kijijini kwao.
Muswada huu unaweza kuwekwa katika mazingira ya kijijini, mahali ambapo maji safi na salama ni tatizo, na ambapo wanakijiji hawajapata msaada wowote kutoka serikalini au katika mashirika yasiyo ya kiserikali na ambapo sasa wanalazimika kutumia juhudi binafsi kutatua tatizo la maji kijijini kwao.
Muswada huu unatokana na mahojiano ya kweli, yaliyofanywa kwa kiongozi mmoja wa kijiji nchini Tanzania. Ili kuutumia vizuri muswada huu katika kituo chako cha redio, unaweza kutumia msanii, kuwakilisha mwenyekiti wa kijiji, na kubadilisha maneno katika muswada ili yaende sambamba na mazingira yenu. Kama utafanya hivyo, tafadhali hakikisha umwewaambia wasikilizaji mwanzoni mwa kipindi kuwa sauti hizo ni za waigizaji, na kwamba kipindi hiki kimewekwa katika mazingira maharia, yenye msingi wa mahojiano halisi.
Script
Piga kiashirio cha kipindi kwa sauti ya chiniAcknowledgements
Washiriki: Emmanuel na Lillian Manyuka, Radio Maria, Tanzania, washirika wa redio ya Farm Radio International.
Imepitiwa na: Alan Etherington, mshauri binafsi wa maji, na uhamasishaji usafi na aliyekuwa mfanyakazi wa shirika la misaada la maji.
Information sources
Mahojiano na viongozi wa kamati ya maji
Shukrani za dhati kwa taasisi ya Harbinger kwa kutoa muswada huu unaohusiana na maji salama.