Unaangalia maandishi ya redio kuhusu Kilimo

Matangazo ya Redio kuhusu kilimo cha ikolojia nchini Tanzania

Oktoba 26, 2022

Tangazo #1: Kutumia pembejeo za Kilimo ikolojia   MSIMULIZI: Wakulima! Ili kupata mavuno mengi na kuimarisha mazingira ya shamba lako kwa wakati mmoja, ni muhimu kujua jinsi ya kuandaa pembejeo za kilimo ikolojia. Hapa kuna vidokezo vitano! Kwanza, pata taarifa zote zinazowezekana kuhusu pembejeo za kilimo unazohitaji. Pili, tafiti vyanzo vyote vinavyowezekana vya mbegu za…

Kuchagua mbegu na kuzihifadhi kwa msimu ujao kwa kuzingatia kanuni za kilimo

Oktoba 4, 2022

SFX: SAUTI YA JUU HALAFU YA CHINI MTANGAZAJI: Mabibi na mabwana, karibuni katika kipindi cha leo, ambapo tutakwenda kujifunza kuhusu kuchagua na kuhifadhi mbegu za msimu ujao kwa mbinu za kilimo. Ili kulizungumzia hili, nilimtembelea Bwana Emmanuel Kakore, mkulima anayeishi kijiji cha Kisiwani, Wilaya ya Same katika Mkoa wa Kilimanjaro, kaskazini mwa Tanzania. Emmanuel Kakore…

Kutatua changamoto za mmomonyoko na uharibifu wa udongo huko Karatu, Tanzania

Julai 21, 2022

MTANGAZAJI: Habari za asubuhi, wasikilizaji. Katika programu ya leo, tutajadili jinsi mmomonyoko na uharibifu wa udongo umeharibu ardhi ya kilimo na kuathiri uzalishaji wa kilimo kwa wakulima wadogo katika wilaya ya Karatu nchini Tanzania. Wilaya ya Karatu iko katika mkoa wa Arusha, kaskazini mwa Tanzania. Pia tutajadili hatua zilizochukuliwa ili kukabiliana na matatizo hayo na…

Taarifa za Awali: Faida za upandaji wa Mazao mbalimbali kwa njia ya mseto

Juni 3, 2022

Utangulizi   Kwa nini somo hili ni muhimu kwa wasikilizaji? Kwasababu wakulima wadogo wanapaswa kufahamu: Jinsi kulima baadhi ya mazao pamoja (kilimo mseto) kunaweza kuongeza mavuno yao. Ni mazao gani ambayo yanaweza kupandwa pamoja bila kuingilia ukuaji na ukomavu wa kila moja, kwa mfano mazao ya mahindi na mikunde. Pia kuna maelewano kati ya mahindi…

Athari za COVID-19 juu ya upatikanaji wa mboga zilizotolewa shambani na jinsi wakulima na wengine wanavyokabiliana na athari hizi

Oktoba 22, 2020

SFX: SIMU INAITA KAMBOLE: Halo, mimi ni Kambole Kanyanta katika Ofisi ya Kilimo ya Wilaya. Naweza kujua ni nani anayepiga simu? FILIUS: Jina langu ni Filius Chalo Jere, mtayarishaji wa kipindi cha redio cha Kilimo ni Biashara kutoka Breeze FM. Naweza kufanya mahojiano na wewe kwa njia ya simu? KAMBOLE: Vipi kuhusu? FILIUS: Kuhusu athari…

Taarifa za awali: Jinsi ya kuhifadhi chakula vizuri kwa muda mrefu

Agosti 7, 2020

Utangulizi: Kutokana na kuzuiwa watu kutembea katika nchi nyingi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kwa sababu ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19), masoko mengi ya vyakula halisi yamefungwa au kuzuiwa. Hii inathiri wachuuzi, wafanyabiashara, na watumiaji. Wakati, hadi sasa, minyororo ya thamani ya nafaka na kunde haijaathiriwa sana, watumiaji hawawezi kupata chakula halisi…

Utangulizi katika kuthibiti magonjwa ya mifugo: Ugonjwa wa mfumo wa hewa na ugonjwa wa kuhara damu

Julai 3, 2019

Utangulizi:   Je ni kwanini somo hili ni muhimu kwa wasikilizaji? Ili wakulima wajue jinsi ya kujihami na ugonjwa wa kuhara damu na ugonjwa wa mfumo wa hewa. Ili wakulima weweze kugundua dalili za ugonjwa wa kuhara damu na ugonjwa wa mfumo wa hewa kwenye mifugo yao na kugundua mifugo iliyoathirika na magonjwa hayo. Ili…

Wakulima hutumia njia za asili na viatilifu katika kuthibiti wadudu wa mahindi magharibi mwa Tanzania

Machi 30, 2019

MTANGAZAJI: Karibu katika kipindi chako cha leo cha wakulima. Leo, tutakua tukizungumza na wakulima kutoka katika wilaya ya Karagwe, mkoa wa Kagera Magharibi mwa Tanzania. Tutazungumza na wakulima wa mahindi kuhusiana na wadudu wanaoharibu ama kushambulia mahindi yao na hatua mbali mbali ambazo walizichukua katika kukabiliana na wadudu hao. (KIMYA) Ni takribani kilomita 30 kutoka…

Wanawake wakulima watumia mbinu za asili kupambana na wadudu na magonjwa ya maharagwe

Machi 23, 2019

PANDISHA MUZIKI WA UTANGULIZI KISHA PUNGUZA USIKIKE CHINI YA MANENO BW. ENOS: Mabibi na Mabwana, karibu katika kipindi chetu cha leo ambapo tutajifunza jinsi wakulima wanawake katika Mkoa wa Kigoma Magharibi mwa nchi ya Tanzania wanavyopambana na matatizo ya wadudu na magonjwa katika maharagwe kwa kutumia mbinu za asili. Ili kuzungumza juu ya hilo, niliwatembelea…

Taarifa za kina: Kupunguza upotevu wa mahindi baada ya mavuno

Novemba 4, 2018

  Kwa nini mada hii ni ya muhimu kwa wasikilizaji? Kwasababu wakulima wa mahindi, wafanyabiashara na wasindikaji wanapaswa kujua: Jinsi gani ya kutunza mahindi baada ya kuvuna na kuepuka upotevu na kuepuka kushambuliwa na wadudu. Vifaa sahihi vya kuvunia. Muda muafaka wa kuvuna mahindi. Namna gani ya kukausha mahindi ipasavyo kuepeuka kushambuliwa na fangasi na…