Ujumbe kwa mtangazaji
Taarifa kwa Mtangazaji
Mlo uliotengenezwa nyumbani wenye lishe kamili unaopatiwa kuku wa kienyeji huboresha ubora na ladha ya kuku wa kienyeji, huwafanya wapendwe na wateja, na huunda nafasi thabiti ya soko kwa wale wanaofuga kuku. Hii inasaidia kufanya kuku wa kienyeji kuwa maarufu zaidi katika masoko ya Tanzania kuliko kuku wa kisasa.
Soko kwa ajili ya kuku na mayai ya kienyeji nchini Tanzania ni bora zaidi kuliko soko la kuku wa kisasa, kwani walaji wanapendelea kuku wanaokula chakula cha asili au kienyeji, kuliko wale wanaolishwa mchanganyiko wa vyakula vya viwandani vilivyochanganywa na madawa.
Mwongozo huu utakusaidia kuelewa jinsi wafugaji wa kuku wa kienyeji kutoka Mkoa wa Dodoma wanavyoandaa chakula cha kuku wa kienyeji. Kuwalisha kuku wao kwa vyakula vinavyopatikana kwenye maeneo yao, kunawasaidia wafugaji kupambana na umasikini na kujipatia kipato kwenye kaya.
Mwongozo huu unatokana na mahojiano halisi. Unaweza kuutumia kuandaa maelezo kwenye mada kama hiyo katika mkoa wako. Unaweza pia kutumia waigizaji wa sauti kuwasilisha muongozo huu kwenye kituo chako cha redio. Ukifanya hivyo, tafadhali waambie wasikilizaji wako mwanzoni mwa kipindi cha redio kuwa hizi ni sauti za waigizaji na sio sauti za wahojiwa halisi.
Kama ungependa kuunda vipindi kuhusu ufugaji wa kuku wa kienyeji, unaweza kuwahoji wafugaji wadogo wadogo na wataalamu wa ufugaji wa kuku katika eneo lako. Unaweza kufikiria kuwauliza maswali yafuatayo:
- Njia bora ya kulisha kuku wa kienyeji ni ipi? Je, lishe inapaswa kuwa tofauti kwa kuku wadogo na wakubwa?
- Wakulima wanapaswa kuwalinda vipi kuku wa kienyeji dhidi ya magonjwa?
- Wakulima wanawezaje kujenga mabanda yanayofaa ili kufuga kuku wa kienyeji kwa usalama na kuwafanya wawe na afya?
Script
Iwe nyama ya kuku wa kienyeji inatumika kupikwa kwenye mchuzi, kuchomwa au kuokwa, haihitaji vihifadhi au viungo vingi ili iwe na ladha nzuri. Inapendwa sana kiasi kwamba wakati mwingine watu husafiri umbali mrefu kupata nyama au mayai wanayoyapenda. Hili ni kweli hasa kwa watu wengi wanaoishi katika maeneo ambapo kuku wa kisasa ndio wanapatikana kwa wingi. Watu wengi wanafahamu kuwa kuku wa kienyeji hula vyakula vinavyopatikana katika mazingira ya asili yanayowazunguka, na kwamba hali hii husababisha upatikanaji wa nyama na mayai yenye ubora wa hali ya juu. Leo, tutaangalia jinsi wakulima wanavyoweza kuandaa chakula cha kuku wa kienyeji.
Katika kipindi hiki, tutafanya mahojiano na watu watano. Anna Msenduki ni mtaalamu kutoka ofisi ya kilimo ya Wilaya ya Mpwapwa, Mkoa wa Dodoma. Pia tuna wakulima watatu kutoka kijiji cha Hogoro katika Wilaya ya Kongwa: Petro, Silvester Gidion, na Juktani Simon. Aidha, tutazungumza na Veronika Masaka, mkulima kutoka Mkoa wa Dodoma, katikati mwa Tanzania. Mabibi na mabwana, mnakaribishwa sana.
Veronica Masaka ni mfugaji wa kuku wa kienyeji ambaye atazungumzia jinsi anavyowalisha kuku wake wa kienyeji.
Kila mara ninahakikisha kuna maji ya kutosha nje ya banda. Kwa njia hii, wanapohitaji maji, wanaweza kuyapata kwa urahisi badala ya kukaa muda mrefu pasipo kunywa maji au kunywa maji machafu na/au yaliyochafuliwa ambayo yanaweza kusababisha magonjwa.
Wanapotoka kwenye banda saa kumi na mbili asubuhi Jumatatu, nawapa chakula kidogo cha mabaki ya chakula kwenye bakuli lao la chakula.
Baada ya hapo, nawaruhusu waende kutafuta vyanzo vingine vya lishe wenyewe nnje kwa sababu kuna vyanzo vingi vya wao kupata chakula katika eneo la karibu hadi wanaporudi kwenye banda lao jioni.
Matunda hutoa virutubisho mbalimbali kama vile vitamini C vinavyowalinda dhidi ya magonjwa.
Yanaweza kuwa mapera, ndizi, au matunda mengine tofauti. Kuku wanapenda matunda kila mara na huwa wanayala na kumaliza kabisa.
Chakula tunachowapa kina virutubisho ambavyo wanavikosa kutoka kwenye chakula ambacho wanajitafutia wenyewe na kinajumuisha mtama na mahindi.
Jioni, tunawaandalia maji ya kunywa na kusafisha makazi yao kwa mara ya pili ili kuhakikisha wanalala mahali safi na salama.
Tunafanya hivi hasa ili kulinda kuku wadogo kutokupata magonjwa kutokana na makazi machafu, na pia kuwalinda wasile uchafu ambao pia unaweza kusababisha magonjwa.
Daima tunawatenga kuku wakubwa na wadogo ili tuweze kuwapa chakula tofauti. Mara nyingi, tunawapa chakula tofauti kuku wadogo na wakubwa, hasa wale walioko kwenye mabanda tuliyojenga.
Mabanda ya vyumba yana urefu kuanzia nusu mita hadi mita moja na nusu na upana wa mita tano, na yana vyumba viwili. Vinakuwa na vifaa maalum vya kulisha ambavyo huzuia chakula kumwagika, pamoja na vifaa vya kutoa maji.
Tunafanya usafi wa mabanda kila asubuhi.
Pia, tunatenga kuku wadogo kutoka sehemu ambapo kuku wakubwa wanakaa.
Lishe ya kuku wa kienyeji au wa asili haitofautiani sana na ile ya kuku wa kisasa (chotara). Kwa kawaida, kuku wa asili hufugwa kwa mfumo wa kuachiwa huru, wakati kuku wa chotara hufugwa kwa mfumo wa nusu kufungiwa na nusu kuachiwa, na mara nyingi hufugwa pamoja na kuku wa asili.
Kwa upande wa chakula, aina hizi mbili za kuku hazina tofauti kubwa. Lengo ni kuwafuga kibiashara, hivyo tunataka wakue haraka na wapate virutubisho sahihi. Kwa mfano, chakula cha kuku kinaweza kujumuisha mtama, uwele, chokaa, madini yaliyochanganywa tayari, mashudu ya mbegu, na chumvi. Hii husaidia kuku kupata virutubisho na madini muhimu kwa ajili ya kujenga miili yao.
Aidha, kwa kuwa kuku hufugwa kwa mfumo wa nusu kufungiwa na nusu kuachiwa, hupata pia wadudu wa aina mbalimbali, ambao huongeza virutubisho muhimu katika mlo wao.
Kwanza, ongeza kilo 25 za pumba za mahindi au mtama; pili, ongeza kilo 44 za mtama au mahindi; tatu, ongeza kilo 17 za mashudu ya mbegu za alizeti, mashudu ya ufuta, mashudu ya pamba, au mashudu ya karanga; nne, ongeza kilo 3.25 za unga wa mifupa au chokaa; tano, ongeza kilo 10 za dagaa au unga wa samaki; sita, ongeza robo kilo ya chumvi ya jikoni; na mwisho, ongeza nusu kilo ya virutubisho. Mchanganyiko huu pia unatoa kilo 100 za chakula.
Kwanza, unaongeza kilo 31 za pumba za mahindi au mtama; pili, ongeza kilo 38 za mashudu ya mbegu za alizeti, mashudu ya ufuta, mashudu ya pamba, au mashudu ya karanga; tatu, ongeza kilo 2.25 za unga wa mifupa au chokaa; nne, ongeza kilo 13 za dagaa au unga wa samaki; tano, ongeza nusu kilo ya chumvi ya jikoni; na sita, ongeza robo kilo ya virutubisho. Hii inatoa jumla ya kilo 100.
Ni muhimu kutambua kwamba mchanganyiko huu wa mwisho ni kwa ajili ya kuku wa kienyeji wanaofugwa kibiashara tu, na hufanya kuku kuwa na mafuta.
Lakini ikiwa unataka kuku wako wa kienyeji wakue haraka kwa mchanganyiko huu, anza kuwapa mwishoni mwa mwezi wa tatu. Baada ya hapo, unapaswa kuwapatia mchanganyiko ufuatao wenye viambato 10 ili kujiandaa kutaga mayai:
Kwanza, kilo 2 za dagaa; pili, kilo 2 za unga wa damu; tatu, kilo 8 za mashudu ya mbegu za ufuta; nne, kilo 5 za pumba za mahindi; tano, kilo 24 za mahindi; sita, kilo 5 za chokaa; saba, kilo 4 za unga wa mifupa; nane, gramu 150 za virutubisho kwa kuku wa mayai; tisa, gramu 50 za methionini; na mwisho, gramu 30 za chumvi.
Katika kipindi hiki, tumeona kwamba wafugaji wanaweza kutumia mabaki ya chakula kuwapatia kuku wa kienyeji kabla ya kuwaachia kutoka kwenye mabanda yao ili wajitafutie chakula chao wenyewe.
Pia, tumeona kwamba kuku wa kienyeji wanaweza kulishwa mabaki ya matunda au matunda yenyewe.
Zaidi ya hayo, kuku wa kienyeji wanaweza kutumia muda mwingi nje ya mabanda, na wanaweza pia kupewa chakula wakiwa ndani ya banda, ikiwemo majani.
Mwishowe, wafugaji wanaofuga kuku wa kienyeji wanapaswa kuwa na mawasiliano ya karibu na maafisa mifugo ili kuwatarifu pale kuku wao watakapokuwa na matatizo ya magonjwa au kupata ushauri wa kitaalamu.
Acknowledgements
Imeandaliwa na: Method Charles, Mwandishi wa masuala ya Kilimo, Arusha, Tanzania
Imehaririwa na: Eliud M. A. Letungaa. Afisa Kilimo na Mifugo, Mtandao wa Vikundi vya Wakulima na wafugaji Mkoa wa Arusha (MVIWAARUSHA).
Vyanzo vya taarifa
Anna Msenduki, Afisa kilimo, Wilaya ya Mpwapwa, Mkoa wa Dodoma, Alihojiwa July 6, 2022.
Jesca Petro, Mkulima, Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma Region, Alihojiwa July 5, 2022.
Silvester Gidion, Mkulima, Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma, Alihojiwa July 5, 2022.
Juktani Miagi, Mkulima, Wilaya ya Kongwa, Mkoa wa Dodoma, Alihojiwa, July 5, 2022.
Veronika Masaka, farmer, Mvumi, Dodoma Region, interviewed Aug. 9, 2022.
Chanzo hichi kimeandaliwa kwa msaada wa kifedha wa Taasisi ya Biovision.
